sw_tn/isa/48/09.md

798 B

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Kwa ajili ya jina langu nitasitisha hasira yangu

Hapa neno "jina" lina maana ya sifa ya Yahwe. "Kwa ajili ya sifa yangu nitakawiza hasira yangu"

na kwa ajili ya heshima yangu nitajizuia kukuangamiza

Sehemu hii ya sentensi ina maana moja kama sehemu ya kwanza.

Tazama, nilikutakasa, lakinii sio kama fedha; nimekutakasa katika tanuu la mateso

Yahwe anazungumzia kutumia mateso kusafisha watu wake kana kwamba walikuwa vyuma vya thamani na mateso yalikuwa tanuu ambano anawatakasa.

kwa kuwa ninawezaje kuruhusu jina langu kudharauliwa?

Yahwe anatumia swali kusisitiza kuwa hawezi kuruhusu jina lake mwenyewe kudharauliwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa maana sitaruhusu yeyote kudharau jina langu"