sw_tn/isa/47/01.md

963 B

Taarifa ya Jumla

Katika sura hii, Yahwe anazungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

keti katika vumbi, binti bikira wa Babeli; keti juu ya ardhi ... binti wa Wakaldayo.

Misemo hii miwili ina maana moja. Kuketi katika mavumbi ni ishara ya aibu.

binti bikirawa Babeli ... binti wa Wakaldayo

Misemo hii miwili ina maana ya mji, Babeli, ambao unazungumziwa kana kwamba ilikuwa binti. Ya kwamba mji ni "binti" ikionyesha jinsi watu wanavyofikiri kwa kubembeleza juuyake.

bila kiti cha enzi

Hapa "kiti cha enzi" ina maana ya nguvu ya kutawala. "bila nguvu ya kutawala"

Hautaitwa tena mrembo na wa kuvutia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu hawatakuita tena mrembo na wa kuvutia"

mrembo na mzuri

Maneno haya mawili yanatumia maana moja. Wanafafanua yule ambaye ni mzuri na anaishi katika starehe. "mzuri sana" au "mwenye starehe sana"

jiwe la kusaga

jiwe kubwa linatumiwa kusaga nafaka