sw_tn/isa/38/12.md

1.1 KiB

Maelezo yaJumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

Maisha yangu yameondolewa na kubebwa mbali na mimi kama hema la mchungaji

Hii inazungumzia jinsi Yahwe anamaliza uhai wa Hezekia kwa haraka kwa kulinganisha kwa jinsi mchungaji anavyotoa hema lake kutoka ardhini. "Yahwe amechukua uhai wangu kutoka kwangu haraka kama mchungaji anavyopanga hema lake na kulibeba mbali"

Maisha yangu yameondolewa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe amechukua uhai wangu"

Nimekunjua maisha yangu kama mfumaji; unanikata kutoka katika kitanda cha mfumi

Hii inazungumzia Yahwe kumaliza uhai wa Hezekia haraka kwa kulinganisha na jinsi mfumaji hukata nguo yake kutoka katika kitanda cha mfumi na kukikunjua juu. "unamaliza uhai wangu haraka, kama mfumaji anavyokata nguo yake kutoka katika kitnda inapokamilika"

unakata

Hapa "unakata" ni umoja na ina maana ya Mungu.

kitanda cha mfumi

chombo kinachotumika kufuma uzi pamoja kutengeneza nguo.

kama simba anavunja mifupa yangu yote

Hezekia anazungumza jinsi alivyo katika maumivu makala kwa kulinganisha kuwa na mwili wake kuraruriwa na simba. "maumivu yangu ni kana kwamba nimeraruliwa na simba"