sw_tn/isa/35/05.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Mistari hii inaanza maelezo ya utukufu ujao wa watu wa Mungu.

macho ya vipofu yataona

"Vipofu" ina maana ya watu ambao ni vipofu. Wanamaanishwa kwa "macho" yao kusisitiza uponyaji wao. "watu vipofu wataona"

masikio ya viziwi yatasikia

"Viziwi" ina maana wa watu ambao hawawezi kusikia. Wanamaanishwa kwa "masikio" yao kusisitiuza uponyaji wao. "watu viziwi watasikia"

mtu kilema ataruka kama mbawala

Hii ina maana mtu ambaye hawezi kutembea ataweza kuruka. Uwezo wake kuruka inakuzwa kwa kusema ya kwamba anaweza kuruka kama mbawala. "mtu kilema ataruka juu"

ulimi usiozungumza utaimba

Hii ina maana ya watu ambao hawawezi kuongea. Wanamaanishwa kwa "ndimi" zao kusisitiza uponyaji wao. "bubu wataimba"

vijito katika nyika

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "vijito vitatiririka katika nyika"

mchanga unaochoma utakuwa dimbwi

Hii ina maana ya kwamba dimbwi la maji litajitokeza katika mchanga wa moto. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Dimbwi litajitokeza katika mchanga unaochoma"

ardhi yenye kiu

Hapa ardhi kavu inaelezwa kama kuwa na kiu. "ardhi iliyokauka"

ardhi yenye kiu kuwa chemchemi za maji

Hii ina maana ya kwamba chemchemi itajitokeza katika ardhi ngumu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "chemchemi za maji zitatokea katika ardhi yenye kiu"

mbweha

mbwa mwitu

mafunjo na matete

Hii ni mimea ambayo huota katika maeneo yaliyoloana.