sw_tn/isa/35/01.md

1.5 KiB

Nyika na mahali penye ukiwa patafurahi; na jangwa litashangilia

Misemo hii miwili kimsingi iuna maana moja. Sehemu hizi inaelezwa kama kuwa na furaha, kama mtu anavyokuwa na furaha, kwa sababu zimepokea maji na zinachanua. "Itakuwa kama nyika na mahali penye ukiwa pana furaha na jangwa litashangilia"

na kuchanua

Hii inazungumzia mimea katika jangwa kuchanua kana kwamba jangwa lenyewe lilikuwa likichanua. "na mimea yake itachanua"

Kama waridi, litachanua kwa wingi

Hii inalinganisha namna ya mimea ya jangwa huchanua kwa namna ambavyo waridi unavyochanua kwa wingi. "Jangwa litaota mimea na miti mipya mingi"

na kushangilia kwa furaha na kuimba

Hii inazungumzia jangwa kana kwamba ilikuwa na furaha na kuimba kama mtu. "itakuwa kana kwamba kila kitu kinashangilia na kuimba!"

utukufu wa Lebanoni utapewa kwake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Hii inazungumzia Yahwe kulifanya jangwa kuonekana na utukufu kama wa Lebanoni kana kwamba alikuwa akilipa jangwa utukufu wa Lebanoni. "Yahwe ataupatia Lebanoniu utukufu wake" au "Yahwe ataufanya uwe mzuri kama Lebanoni"

uzuri wa Karmeli na Sharoni

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. Pia, hii inamzungumzia Yahwe kulifanya jangwa kuonekana zuri kama Karmeli na Sharoni kana kwamba alikuwa akilipa jangwa uzuri wake. "uzuri wa Karmeli na Sharoni utapewa kwake" au "Yahwe ataufanya uwe mzuri kama Karmeli na Sharoni"

utukufu wa Yahwe, uzuri wa Mungu wetu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja na inasisitiza kutokea kwa Yahwe.