sw_tn/isa/30/06.md

726 B

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza tamko la Mungu kuhusu watu wa Yuda.

tamko

"Hiki ndicho Yahwe anachotamka"

ya simba jike na simba, kipiribao na nyoka mkali anayepaa

Hii ina maana ya aina hawa ya wanyama kwa ujumla. "ambapo simba jike na simba huishi, na ambapo kuna kipiribao na nyoka"

nyoka mkali anayepaa

Hapa neno "mkali" huenda una maana ya sumu ya nyoka anapouma na neno "kupaa" lina maana ya kusogea kwake kwa haraka.

wanabeba utajiri wao

"watu wa Yuda wanabeba utajiri wao"

nimemuita Rahabu, ambaye hukaa kwa kutulia

Kulikuwa na simulizi maarufu kuhusu joka la baharini linaloitwa Rahabu. Jina Rahabu ina maana ya "nguvu" au "kiburi". "Ninaita Misri mwenye kiburi wa sauti ambaye hafanyi lolote"