sw_tn/isa/21/01.md

1.5 KiB

Tamko

"Hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "Huu ni ujumbe wa Yahwe"

kuhusu jangwa karibu na bahari

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi babeli kama kuwa jangwa, ingawa Mungu bado hajapafanya kuwa jangwa. Tukio hili hakikalitatokea. "kuhusu watu wanaoishi katikanchi ambayo punde itakuwa jangwa"

Kama upepo wa dhoruba unavyofyeka katikati ya Negebu

Isaya analinganihsa jeshi ambalo litashambulia watu na dhoruba yenye upepo mkali. Watakuwa na kasi na nguvu.

kutoka nyikani

Hapa "nyikani" ina maana ya nyika ya Yuda.

kutoka katika nchi ya kutisha

Jeshi linatokana na watu ambao husababisha hofu kubwa.

maono ya kudhihikisha yameletwa kwangu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe alinionyesha maono ya kusumbua akili"

mwanamume mdanganyifu anafanya udanganyifu

"wale wanaodanganya watadanganya"

na mharibifu huharibu

"na wale wanaoharibu wataharibu"

Nenda juu na ushambulie, Elamu; izingire, Umedi

Katika maono yaliyopatiwa Isaya, Yahwe anazungumza kwa majeshi ya Elamu na Umedi kana kwamba walikuwa wakimsikiliza.

Nenda juu na ushambulie, Elamu; izingire, Umedi

Inaeleweka ya kwamba wanapaswa kushambulia Wababeli. "Nenda juu na ushambulie Wababeli, nyie wanajeshi wa Elamu; nendeni na muwazingire Wababeli, nyie wanajeshi wa Umedi"

Elamu ... Umedi

Hapa "Elamu" na "Umedi" inawakilisha wanajeshi kutoka maeneo haya.

Nitakomesha minung'uniko yake yote

Hapa "yake" inawakilisha watu wote ambao wanateseka kwa sababu ya Wababeli. Yahwe atasababisha kuacha kulalamika atakapotuma majeshi ya elamu na Umedi kuangamiza Wababeli.