sw_tn/isa/18/04.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla

Mungu anatumia fumbo kuhusu mkulima katika shamba la mizabibu ili kufafanua kile atakachofanya kwa taifa fulani. Taifa hilo ni kati ya Kushi au adui wa Kushi.

Hiki ndicho Yahwe alichosema kwangu

"Yahwe aliniambia". Hapa neno "kwangu" ina maana ya Isaya.

Nitachunguza kwa utulivu kutoka kwenye nyuma yangu

Kile Mungu atakachochunguza kinaweza kuwekwa wazi. "Nitachunguza taifa hilo kwa utulivu kutoka nyumbani kwangu" au "Kutoka nyumbani kwangu, nitatazama kwa utulivu kile ambacho watu wa taifa hilo wanachofanya"

kama joto linalochemka pole pole katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la mavuno

Misemo hii inaonyesha jinsi gani Mungu atazama taifa kwa utulivu.

Kabla ya mavuno

"Kabla ya mavuno ya zabibu"

pale ambapo uchanuzi umekamilika

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba hii ina maana ya kuchanuka juu ya mizabibu. "pale ambapo maua yamekamilisha kuota juu ya mizabibu"

atayakata matawi

Kama mkulima anaona ya kwamba tawi jipya halizai tunda, atalikata. "mkulima atakata matawi ambayo hayazai matunda"

makasi ya kupogolea

Mkasi wa kupogolea ni kisu ambacho watu hutumia kukata matawi katika mizabibu au mimea mingine.

atakata chini na kuondoa matawi yaliyotawanyika

Kama mkulima anaona ya kwamba tawi limeota sana na linafanya mzabibu wote kutozaa matunda mengi, ataukata na kuutupa.