sw_tn/isa/13/01.md

973 B

kuhusu Babeli

Jina la mji lina maana ya watu wa Babeli. "kuhusu watu wa Babeli"

Amozi

Amozi alikuwa baba wa Isaya.

lia kwa sauti kwao

Neno "kwao" ina maana ya wanajeshi kutoka nchi nyingine.

malango ya waadilifu

Maana zaweza kuwa 1) "malango ya Babeli ambapo waadilifu wanaishi" au 2) "malango ya nyumba kubwa za waadilifu"

waadilifu

"watu wanaoheshimiwa" au "watawala"

watakatifu wangu

"wale ambao nimewaweka kando kwa ajili yangu" au "jeshii ambalo nimeliweka kando kwa ajili yangu"

Nmewaita wanamume wangu wenye uwezo kutekeleza hasira yangu

Kutekeleza hasira ya Mungu inawakilisha kuadhibu watu kwa sababu ya hasira ya Mungu. "Nimewaita wanajeshi wenye nguvu kuadhibu watu wa Babeli kwa sababu wamenikasirisha"

hata wanaoshangilia kwa kujisifu

"hata wale ambao wanashangilia kwa majivuno". Sababu ya wao kushangilia kwa majivuno inaweza kuwekwa wazi. "hata watu wangu ambao hushangilia kwa majivuno kwa sababu ya mambo makubwa nayofanya"