forked from WA-Catalog/sw_tn
28 lines
989 B
Markdown
28 lines
989 B
Markdown
# Taarifa ya Jumla
|
|
|
|
Hapa Isaya anaendelea kuelezea jinsi itakavyokuwa pale mfalme ambaye Mungu amemchagua anatawala.
|
|
|
|
# Katika siku hiyo
|
|
|
|
Inaweza kuwekwa wazi ni wakati gani unaomaanishwa. "Katika kipindi hicho" au "Pale mfalme anapotawala"
|
|
|
|
# hasira yako imegeuka
|
|
|
|
Hasira ya Mungu inazungumziwa kana kwamba mtu anaweza kugeuka na kuondoka. Ina maana ya kwamba Mungu ameacha kuwa na hasira. "Hauna hasira na mimi tena"
|
|
|
|
# Mungu ni wokovu wangu
|
|
|
|
Mungu anasababisha wokovu wa mtu inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa huo wokovu. Nomino dhahania "wokovu" inaweza kuelezwa na nomino "mwokozi" au kitenzi "okoa". "Mungu husababisha wokovu wangu" au "Mungu ni mwokozi wangu" au "Mungu ndiye anayeniokoa"
|
|
|
|
# Yahwe ni nguvu yangu
|
|
|
|
Mungu kusababisha mtu kuwa na nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa nguvu yao. "Yahwe hunifanya niwe na nguvu"
|
|
|
|
# na wimbo
|
|
|
|
Neno "wimbo" hapa linawakilisha kile mtu anachokiimba. "na yule ambaye nayemwimba kwa furaha"
|
|
|
|
# Amekuwa wokovu wangu
|
|
|
|
"Ameniokoa"
|