sw_tn/isa/12/01.md

989 B

Taarifa ya Jumla

Hapa Isaya anaendelea kuelezea jinsi itakavyokuwa pale mfalme ambaye Mungu amemchagua anatawala.

Katika siku hiyo

Inaweza kuwekwa wazi ni wakati gani unaomaanishwa. "Katika kipindi hicho" au "Pale mfalme anapotawala"

hasira yako imegeuka

Hasira ya Mungu inazungumziwa kana kwamba mtu anaweza kugeuka na kuondoka. Ina maana ya kwamba Mungu ameacha kuwa na hasira. "Hauna hasira na mimi tena"

Mungu ni wokovu wangu

Mungu anasababisha wokovu wa mtu inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa huo wokovu. Nomino dhahania "wokovu" inaweza kuelezwa na nomino "mwokozi" au kitenzi "okoa". "Mungu husababisha wokovu wangu" au "Mungu ni mwokozi wangu" au "Mungu ndiye anayeniokoa"

Yahwe ni nguvu yangu

Mungu kusababisha mtu kuwa na nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa nguvu yao. "Yahwe hunifanya niwe na nguvu"

na wimbo

Neno "wimbo" hapa linawakilisha kile mtu anachokiimba. "na yule ambaye nayemwimba kwa furaha"

Amekuwa wokovu wangu

"Ameniokoa"