sw_tn/isa/09/11.md

902 B

Kwa hiyo Yahwe atamuinua dhidi yake Resini, mshindani wake

Hapa "Resini" inawakilisha jeshi lake. "Kwa hiyo, Yahwe atamleta Resini na jeshi lake dhidi ya watu wa Israeli"

Resini

Hili ni jina la mwanamume.

na atawatikisa maadui zake

Msemo "tikisa" ni lahaja ambayo ina maana ya kuwachochea kushambulia. "na Yahwe atasababisha adui wa Israeli kushambulia"

Watameza Israeli kwa mdomo wazi

"Kumeza" ni jinsi ambavyo wanyama pori hula mawindo. "Kama mnyama mwitu anavyokula mawindo yake, jeshi la adui litaangamiza watu wa Israeli"

Katika vitu hivi vyote, hasira yake haipungui; badala yake, mkono wake

"Hata kama vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu ambaye anataka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuadhibu Israeli. "atakuwa tayari kuwaadhibu"