sw_tn/isa/07/01.md

1.3 KiB

Katika siku za Ahazi ... mfalme wa Yuda

"Pale Ahazi... alipokuwa mfalme wa Yuda" Huu ulikuwa wakati matukio yalitokea.

Resini ... Peka ... Remalia

majina ya wanaume.

Resini ... na Peka ... alikwenda juu

Mwandishi anazungumza kana kwamba wafalme walikuwa majeshi walioyaongoza. "Resini ... na Peka ... waliongoza majeshi yao juu"

kufanya vita dhidi yake

Mwandishi anazungumza kana kwamba mji wenyewe ulikuwa watu ambao huishi ndani yake. "kupiga vita dhidi ya watu wa Yerusalemu"

Ikasemekana katika nyumba ya Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nyumba ya Daudi ikasikia taarifa" au "mtu alitoa taarifa kwa nyumba ya Daudi"

nyumba ya Daudi

Neno "nyumba" ni mfano wa maneno kwa ajili ya familia inayoishi katika nyumba. "Mfalme Ahazi na washauri wake"

ya kwamba Aramu alishirikiana na Efraimu

Hapa "Aramu" na "Efraimu" wanatambua wafalme wao. Efraimu anatumiwa hapa kumaanisha ufalme mzima wa kaskazini wa Israeli. "ya kwamba Resini, mfalme wa Aramu alikuwa akimsaidia Peka, mfalme wa Israeli"

Moyo wake ulitetemeka, na moyo wa watu wake, kama miti ya msituni inavyotetemeka katika upepo

Kutetemeka kwa mioyo yao katika habari hii inalinganishwa na namna miti hutikisika pale upepo unapovuma katikati yao. "Ahazi na watu wake waliogopa sana"