sw_tn/isa/05/05.md

981 B

Taarifa ya Jumla

Katika fumbo hili, mmiliki wa shamba la mizabibu anaendelea kuzungumza juu ya shamba lake la mizabibu.

ondoa kitalu

"ondoa mpaka wa vichaka". Kitalu ni safu ya vichaka au miti midogo ambayo ilipandwa ili kulinda bustani au eneo lingine lolote. Hapa "kitalu" huenda ina maana ya vichaka vya miiba ambavyo vilipandwa kuota katika ukuta wa mawe unaozunguka shamba la mizabibu.

nitaibadili kuwa malisho

"nitaruhusu wanyama kwenda pale na kula". Hili ni eneo lenye nyasi ambapo wanyama hula.

itakanyagwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wanyama watapakanyaga chini"

nitailaza kuwa takataka

"nitapaangamiza"

haitapogolewa wala kupaliliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atapapunguza au kupapalilia" au "hakuna mtu atapakata matawi ambayo hayahitajiki, na hakuna mtu wa kutunza udongo"

mbigili na miiba itachipua juu

Mbigili na miiba mara kwa mara hutumika kama alama za miji na nchi zilizoharibiwa.