sw_tn/isa/02/17.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

Kiburi cha mtu kitashushwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Atawashusha chini watu wenye kiburi" au "Atamuwaibisha kila mwanamume mwenye kiburi"

Kiburi cha wanamume kitaanguka

Nomino dhahania "kiburi" inaweza kutafsiriwa kama kivumishi. "wale watu ambao wana kiburi na wataacha kuwa na kiburi"

Yahwe pekee ayainuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamsifu Yahwe tu"

Hizo sanamu zitapita mbali kabisa

"Sanamu zote zitatoweka" au "Hapatakuwa na sanamu zaidi"

Wanamume watakwenda ... kutoka kwa hofu kuu

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Wanamume watakwenda .. kujificha kutoka kwa hofu kuu"

mapango ya mawe

"mapango katika mawe". Haya ni mawe makubwa, sio mawe madogo ambayo yanaweza kushikiliwa katika mkono.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe, na kutoka kwa utukufu wa ukuu wake wa enzi

Hapa nomino dhahania "hofu kuu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuogofya". "kutoka kwa uwepo wa kuogofya wa Yahwe" au "Kutoka kwa Yahwe kwa sababu utamwogopa sana"

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

kwa sababu walikuwa wanamuogopa sana Yahwe

kutoka kwa utukufu wa ufalme wake

Hapa neno "utukufu" kufafanua "ufalme". "uzuri ambao anao kama mfalme"

atakapoinuka kuogofya dunia

"pale Yahwe atakapochukua hatua na kusababisha watu wa dunia kumuogopa sana"