sw_tn/hos/08/06.md

562 B

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga

Kupanda upepo ni kitendo cha kufanya jambo kwa njia zisizofaa. Kuvuna kimbunga ni kuteseka kutokana na matendo ya mtu mwenyewe.

Mbegu zilizosimama hazina vichwa

Hapa "kichwa" ni sehemu ya mmea mbayo mbegu zinakuwepo. Mmea ambao hauna kichwa unakuwa hauna chochote cha kumpa mkulima. Matendo ya Waisraeli hayatawapa matokeo mazuri.

Ikiwa itakomaa, wageni watakula.

Ikiwa matendo yoyote ya Waisraeli yatasababisha matokeo mazuri basi adui wa Israeli watayachukua.