sw_tn/hos/02/02.md

1.1 KiB

Taarifa ya jumla

Bwana anazungumza na Hosea.

Mashtaka

Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.

Mama yako

Hapa "mama" inamaanisha taifa la Israeli.

kwa kuwa yeye si mke wangu

Bwana anaeleza kuwa Israeli inazungumzwa kama mwanamke ambaye hatendi kama mke kwa Bwana. Badala yake Israeli amegeuka na kuacha kumfuata na kumwabudu yeye.

wala mimi si mumewe

Bwana hawezi kuendelea kuwa na uhusiano na taifa la Israeli kama mume kwa mke wake.

na matendo yake ya uzinzi

Mke ambaye ni mzinzi anamuacha mume wake na kulala na mwanaume mwingine. Hivi ndivyo Israeli alivyofanya mbele ya Bwana.

kati ya matiti yake

Israeli wanategemea miungu na sio Bwana.

nitamvua nguo na kumuonyesha uchi wake kama siku aliyozaliwa

Bwana hataendelea kuwalinda na kuwasaidia Israeli kwa sababu taifa limemwacha.

nitamfanya kama jangwa

Bwana ataibadilisha Israeli ifanane na jangwa ambao nii mji usiozalisha.

nitamfanya afe kutokana na kiu

Hapa "kiu" inamaana ya uhitaji wa kumwabudu Bwana na sio miungu mingine, au Israeli hawatatweza kuishi kama taifa.