1.1 KiB
Taarifa ya jumla
Bwana anazungumza na Hosea.
Mashtaka
Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.
Mama yako
Hapa "mama" inamaanisha taifa la Israeli.
kwa kuwa yeye si mke wangu
Bwana anaeleza kuwa Israeli inazungumzwa kama mwanamke ambaye hatendi kama mke kwa Bwana. Badala yake Israeli amegeuka na kuacha kumfuata na kumwabudu yeye.
wala mimi si mumewe
Bwana hawezi kuendelea kuwa na uhusiano na taifa la Israeli kama mume kwa mke wake.
na matendo yake ya uzinzi
Mke ambaye ni mzinzi anamuacha mume wake na kulala na mwanaume mwingine. Hivi ndivyo Israeli alivyofanya mbele ya Bwana.
kati ya matiti yake
Israeli wanategemea miungu na sio Bwana.
nitamvua nguo na kumuonyesha uchi wake kama siku aliyozaliwa
Bwana hataendelea kuwalinda na kuwasaidia Israeli kwa sababu taifa limemwacha.
nitamfanya kama jangwa
Bwana ataibadilisha Israeli ifanane na jangwa ambao nii mji usiozalisha.
nitamfanya afe kutokana na kiu
Hapa "kiu" inamaana ya uhitaji wa kumwabudu Bwana na sio miungu mingine, au Israeli hawatatweza kuishi kama taifa.