sw_tn/heb/13/intro.md

919 B

Waebrania 13: Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Mwandishi anamalizia orodha ya mashauri aliyoyaanza katika sura ya 12. Halafu anawauliza wasomaji wake kumuombea anapomalizia barua hii.

Watafsiri wengine wametenga kila mistari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 13:6 ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Ukarimu

Mungu anataka watu wake wakaribishe watu wengine kuja kwa nyumba zao kula chakula na hata kulala. Watu wake wanastahili wafanye hivi hata kama hafahamu vizuri watu wanaowaalika. Katika Agano la Kale, Abrahamu na binamu yake Lutu walionyesha ukarimu kwa watu ambao hawakuwafahamu. Abrahamu aliandaa chakula cha bei na Lutu akawakaribisha kulala kwake.Walikuja kufahamu baadaye kwamba watu hao walikua malaika.

__<< | __