sw_tn/gen/44/30.md

1.8 KiB

Kwa hiyo

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika hapa kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

basi, nitapokuja ... huzuni ya kuzimu

Yuda anaelezea kwa Yusufu suala la ukweli lakini la kubuni ambalo linatarajiwa kutokea kwa Yakobo atakaporudi bila Benyamini.

nitapokuja kwa mtumishi wako

Hapa "nitakapokuja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda" au "kurudi".

kijana hayupo nasi

"kijana hayupo pamoja nasi"

kwa kuwa uhai wake umefungamanishwa katika uhai wa kijana

Baba anasema ya kwamba atakufa iwapo mwanawe atangekufa inazungumziwa kana kwamba maisha yao mawili yaliunganishwa pamoja kimwili. "kwa maana alisema angekufa iwapo kijana hangerudi"

itakuwa

Yuda anazungumzia kuhusu suala la kubuni katika wakati wa mbele kana kwamba ingetokea kweli.

watumishi wako watazishusha mvi za mtumishi wako baba yetu kaburini kwa masikitiko

"watazishusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"

watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Nasi, watumishi wako" au " Na sisi"

mvi za mtumishi wako baba yetu

Hapa "mvi" ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "baba yetu mzee"

Kwani mtumishi wako alikuwa mdhamini wa kijana kwa baba yangu

Nomino hii inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "aliahidi". "Maana nimuahidi baba yangu kuhusu kijana huyu"

Kwani mtumishi wako

Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". "Kwa maana mimi, mtumishi wako" au "Kwa maana mimi"

ndipo nitakapokuwa mwenye hatia kwa baba yangu

Kuchukuliwa mwenye hatia inazungumziwa kana kwamba "hatia" ilikuwa kitu ambacho mtu hubeba. "kisha baba yangu anaweza kunilaumu"