sw_tn/gen/44/20.md

1.3 KiB

Maelezo ya Jumla:

Yuda anaendelea kuzungumza mbele ya Yusufu.

Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Tunaye baba ... baba yake anampenda.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nasi tukamwambia bwana wetu ya kwamba tuna baba ... baba yake anampenda"

tukamwambia bwana wangu

Yuda anamtambua Yusufu kama "bwan wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. "tulisema kwako, bwana wangu"

baba yake anampenda

Hii ina maana ya upendo kwa rafiki au mmoja wa familia.

Nawe ukawambia watumishi wako, 'Mleteni ili nimwone.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nawe ukasema kwa mtumishi wako ya kwamba tunapaswa kumleta ndugu yetu mdogo kwako ili uweze kumuona"

Nawe ukawambia watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". "Kisha ulisema kwetu, watumishi wako"

Mleteni ili nimwone

Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" pale ilipozungumziwa safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri. "Mleteni kwangu"

Baada ya hapo, tukamwambia bwana wangu, 'Kijana hawezi ... baba yake angekufa.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kwa kujibu, tulisema kwa bwana wangu ya kwamba kijana hawezi ... baba yake angekufa"

baba yake angekufa

Inadokezwa ya kwamba baba yao angekufa kwa huzuni.