sw_tn/gen/43/03.md

1.0 KiB

Yuda akamwambia

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

Yule mtu

Hii ina maana ya Yusufu, lakini ndugu hawakujua alikuwa Yusufu. Walimtaja kama "mtu" au "yule mtu, bwana wa nchi" kama katika 42:29.

alituonya, "Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

alituonya kwa ukali

"alikuwa na hali ya ukali alipotuonya, akisema"

Hamtauona uso wangu

Yuda anatumia msemo huu mara mbili katika 43:3-5 kuweka msisitizo kwa baba yake ya kwamba hawawezi kurudi Misri bila Benyamni. Msemo "uso wangu" una maana ya yule mtu, ambaye ni Yusufu. "Hamtaniona"

ndugu yenu awe nanyi

Yuda ana maana ya Benyamini, mtoto wa Raheli wa mwisho kabla yeye hajafa.

hatutashuka

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.