forked from WA-Catalog/sw_tn
28 lines
1.0 KiB
Markdown
28 lines
1.0 KiB
Markdown
|
# Yuda akamwambia
|
||
|
|
||
|
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"
|
||
|
|
||
|
# Yule mtu
|
||
|
|
||
|
Hii ina maana ya Yusufu, lakini ndugu hawakujua alikuwa Yusufu. Walimtaja kama "mtu" au "yule mtu, bwana wa nchi" kama katika 42:29.
|
||
|
|
||
|
# alituonya, "Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi"
|
||
|
|
||
|
Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"
|
||
|
|
||
|
# alituonya kwa ukali
|
||
|
|
||
|
"alikuwa na hali ya ukali alipotuonya, akisema"
|
||
|
|
||
|
# Hamtauona uso wangu
|
||
|
|
||
|
Yuda anatumia msemo huu mara mbili katika 43:3-5 kuweka msisitizo kwa baba yake ya kwamba hawawezi kurudi Misri bila Benyamni. Msemo "uso wangu" una maana ya yule mtu, ambaye ni Yusufu. "Hamtaniona"
|
||
|
|
||
|
# ndugu yenu awe nanyi
|
||
|
|
||
|
Yuda ana maana ya Benyamini, mtoto wa Raheli wa mwisho kabla yeye hajafa.
|
||
|
|
||
|
# hatutashuka
|
||
|
|
||
|
Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.
|