sw_tn/gen/42/23.md

929 B

hawakuja ... mkalimani kati yao

Hii inabadilisha kutoka kwenye simulizi kuu kwenda kwenye taarifa ya nyuma ambayo inaelezea kwa nini ndugu walidhani Yusufu hakuweza kuwaelewa.

mkalimani

"Mkalimani" ni mtu ambaye hutafsiri kile mtu anazungumza katika lugha nyingine. Yusufu aliweka mkalimani kati yake na ndugu zake kufanya ionekane kana kwamba hakuzungumza lugha yake.

Akatoka kwao na kulia

Inasemekana ya kwamba Yusufu alilia kwa sababu alipatwa na hisia baada kusikia walichosema ndugu zake.

kuongea nao

Yusufu aliendelea kuzingumza katika lugha nyingine na kutumia mkalimani kuzungumza na ndugu zake.

kumfunga mbele ya macho yao

Hapa "macho" ina maana ya machoni mwao. "alimfunga machoni mwao" au "alimfunga huku wakitazama"

na kuwapa mahitaji

"kuwapatia mahitaji waliyohitaji"

Wakatendewa hivyo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Watumishi walifanya kwao kila kitu ambachoYusufu aliwaamuru"