sw_tn/gen/40/14.md

617 B

unionesha wema

"na tafadhali unioneshe wema kwangu"

Unitaje kwa Farao na kuniondoa hapa gerezani

Yusufu ana maana ya mnyweshaji kumwambia Farao juu yake ili kwamba Farao amfungulie kutoka gerezani. "Nisaidie kutoka katika gereza hili kwa kumwambia Farao juu yangu"

Maana hakika nilitekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Maana hakika watu walinichukua" au "Maana hakika Waishmaeli walinichukua"

nchi ya Waebrania

"nchi ambayo Waebrania huishi"

hapa sijafanya chochote kinachonipasa niwekwe gerezani

"na pia nilipokuwa hapa Misri, sijafanya jambo lolote ambalo nastahili kuwekwa gerezani"