sw_tn/gen/39/07.md

1.2 KiB

Ikawa baada ya hayo

"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya katika simulizi.

Tazama

"Sikia". Yusufu anatumia neno hili kuvuta nadhari ya mke wa Potifa.

bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani

"bwana wangu hajishughulishi juu ya nyumba yake napokuwa msimamizi." Hii inaweza kuandikwa katika hali ya chanya. "bwana wangu ananiamini na nyumba yake"

ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu

Kitu kinachokuwa "chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu huyo anawajibika kutunza na kulinda. "Kwa hiyo Potifa alimweka Yusufu kuwa mwangalizi wa kila kitu ambacho alikuwa nacho"

Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi

Hapa mwandishi anazungumzia juu ya mamlaka kana kwamba yalikuwa ukubwa. "Nina mamlaka katika nyumba hii kuliko mtu yeyote yule"

Hajanizuia chochote isipokuwa wewe

Hii inaweza kusemwa katika hali ya chanya. "Amenipatia kila kitu isipokuwa wewe"

Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?

Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika siwezi kufanya jambo hili ovu na kutedna dhambi dhidi ya Mungu"