sw_tn/gen/37/29.md

611 B

Rubeni akarudi kwenye shimo, na, tazama, Yusufu hakuwemo shimoni

"Rubeni alirudi kwenye shimo, na akashangazwa kuona ya kwamba Yusufu hakuwepo mle" Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Rubeni alishangazwa kukuta ya kwamba Yusufu aliondoka.

Akararua mavazi yake

Hili ni tendo la mawazo na uchungu mkubwa. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Alikuwa na majonzi mpaka akararua nguo zake"

Kijana yuko wapi? Na mimi, je niende wapi?"

Rubeni anatumia maswali kuweka msisitizo kwa tatizo ambalo Yusufu hapatikani. Hivi vinaweza kuandikwa kama kauli. "Kijana ametoweka! Siwezi kurudi nyumbani sasa!"