sw_tn/gen/26/09.md

1.1 KiB

Abimeleki akamwita Isaka kwake

Yawezekana Abimeleki alimtuma mtu kumwambia Isaka ya kwamba alihitaji kumuona. "Abimeleki alimtuma mtu kumleta Isaka kwake"

Kwa nini ulisema, 'Yeye ni dada yangu?"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "Kwa nini ulisema ya kwamba ni dada yako?"

amchukue

"ili amchukue"

Ni jambo gani hili ulilotufanyia?

Abimeleki alitumia swali hili kumkaripia Isaka. "Haukupaswa kufanya jambo hili kwetu!"

ungeweza kuleta hatia juu yetu

Hii inazungumzia kuhusu kumsababisha mtu kuwa na hatia kana kwamba "hatia" ilikuwa ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "ungeweza kusababisha tuwe na hatia ya kuchukua mke wa mtu"

juu yetu

Hapa "yetu" ina maana ya Abimeleki na watu wake.

Mtu yeyote atakayemgusa mtu huyu

Hapa "atakayemgusa" ina maana ya kumgusa kwa namna ya kumdhuru. "Yeyote atakayemdhuru mwanamume huyu"

hakika atauwawa

Inawezekana Abimeleki alikusudia kumwambia mtu kumuua yeyote ambaye angemdhuru Isaka au Rebeka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitamuua" au "Nitawaamuru wanamume wangu kumuua"