sw_tn/gen/23/17.md

1.1 KiB

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.

Mamre

Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"

shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote

Msemo huu unafafanua kile ambacho mwandishi alimaanisha alipoandika "shamba la Efroni". Halikuwa shamba tu, lakini pia pango na miti katika shamba.

kwa Abraham kwa njia ya manunuzi

"ikawa mali ya Abrahamu alipoinunua" au "ikawa ya Abrahamu baada ya kuinunua"

mbele ya wana wa Hethi

Hapa "mbele ya" ina maana ya watu kutumika kama mashahidi. "pamoja na watu wa Hethi wakitazama kama mashahidi"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

wote waliokuja malangoni pa mji wake

Hii inaeleza ni wana wapi wa Hethi waliomwona Abrahamu akinunua mali ile. "wale wote waliokusanyika langoni mwa mji"

malangoni pa mji wake

Malango ya mji palikuwa pale ambapo viongozi wa mji walikutana kufanya maamuzi muhimu.

mji wake

"mji aliokuwa akiishi". Msemo huu unaonyesha Efroni alikuwa wa mji ule. Haimaanishi ya kwamba aliumiliki.