sw_tn/gen/21/01.md

779 B

Yahwe akamsikiliza Sara

Hapa msemo "kumsikiliza" una maana ya Yahwe kumsaidia Sara kupata mtoto. "Yahwe alimsaidia Sara"

akamzalia Abrahamu mtoto wa kiume

"akamzaa mtoto wa kiume wa Abrahamu"

katika uzee wake

"Abrahamu alipokuwa mzee sana"

katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia

"katika muda haswa ambao Mungu alimwambia ingekuja kutokea"

Abrahamu alimuita mwanawe wa kiume, yule ambaye alizaliwa kwake, ambaye Sara alimzaa, Isaka

"Abrahamu alimuita mtoto wake wa kiume, yule ambaye Sara alimzaa, Isaka" au "Abrahamu alimuita mtoto wao wa kiume Isaka"

Abrahamu akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane

"Mwanae Isaka alipofikisha umri wa siku nane, Abrahamu alimtahiri"

siku nane

"siku 8"

amemwagiza

"alimuamuru Abrahamu kufanya"