sw_tn/gen/17/19.md

918 B

Hapana, Sarai mkeo atakuzalia

Mungu alisema hili kusahisha imani ya Abrahamu juu ya Sarai kupata mtoto.

utamwita jina lake

Neno "utamwita" linamlenga Abrahamu.

Na kwa habari ya Ishmaeli

Maneno "na kwa habari" yanaonyesha ya kwamba Mungu anabadilisha maongezi kuhusu mtoto ambaye angezaliwa na kumuongelea Ishmaeli.

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini kwa kile nachotaka kukuambia"

nitamfanya kuwa na uzao

Hii ni lahaja inayokuwa na maana ya "nitamsababisha awe na watoto wengi"

na kumzidisha maradufu

"na nitamsababisha awe na uzao mwingi"

viongozi wa makabila

"machifu" au "watawala". Hawa viongozi sio wana kumi na mbili na wajukuu wa Yakobo ambao wataongoza makabila kumi na mbili ya Israeli.

Lakini agano langu nitalifanya imara na Isaka

Mungu anarudi kuongelea juu ya agano lako na Abrahamu na kusisitiza ya kwamba atatimiza ahadi yake na Isaka, na sio Ishmaeli.