sw_tn/gen/09/01.md

1.2 KiB

Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi

Hii ni baraka ya Mungu. Alimwambia Nuhu pamoja na familia yake kuzaliana wanadamu wengine kama wao, ili kwamba wawe wengi wa aina yao. Neno "mkaongezeke" linafafanua jinsi gani wanapaswa "kuzaana"

Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai ... na juu ya samaki wote wa baharini

Mwandishi anazungumzia hofu na utisho kana kwamba ni vitu vya mwili ambavyo vingeweza kuwa juu ya wanyama. "Kila mnyama hai ... na samaki wote wa baharini watakua na hofu kubwa sana juu yako"

Hofu na utisho wenu

maneno "hofu" na "utisho" zina maana moja na husisitiza jinsi wanyama walivyokuwa wanaogopa binadamu. "Hofu ya utisho kwako" au "Hofu ya kutisha kwako"

kila mnyama aliye hai juu ya nchi

Hili ni moja kati ya makundi manne ya wanyama ambayo mwandishi ameorodhesha, na sio ufupisho wa wanyama waliosalia atakaowataja hapo baadae

ndege

Huu ni msemo wa jumla kwa vitu vinavyopaa. "wanyama warukao" au "vitu vinavyoruka"

juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi

Hii inajumuisha aina yote ya wanyama.

Vimetolewa katika mikono yenu

Mkono ni lugha mbadala kwa mamlaka ambayo mkono ulikuwa nayo. Hii inaweza kuwa katika hali ya kutenda. "Vimetolewa katika mamlaka yako" au "Nimeviweka chini ya mamlaka yako"