sw_tn/gen/04/10.md

1.1 KiB

umefanya nini?

Mungu alitumia swali la balagha kumkaripia Kaini. Hii yaweza kutafsiriwa kama msemo. "Ulichofanya ni kibaya"

damu ya ndugu yako inaniita mimi

Damu ya Habili ni lugha kwa ajili ya kifo chake, kana kwamba ni mtu anayemwita Mungu kumuadhibu Kaini. "Damu ya ndugu yako ni kama mtu akiniita kumuadhibu yule aliyemuua"

sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhini

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ninakulaani ili usiweze kuotesha chakula kutoka ardhini"

ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako

Mungu anazungumzia ardhi kana kwamba ni mtu awezaye kunywa damu ya Habili. "ambayo imelowa kwa damu ya ndugu yako"

kutoka mikononi mwako

Mungu anazungumzia mkono wa Kaini kana kwamba umemwaga damu ya Habili katika "mdomo" wa ardhi. "iliyomwagwa ulipomuua" au "kutoka kwako"

ilima

Hii inamaanisha kufanya kila liwezekanalo ili mimea iweze kuota vizuri.

haita kuzalia wewe nguvu yake

Ardhi inapewa utu kana kwamba ni binadamu anayepoteza nguvu. "ardhi haitakuzalia chakula cha kutosha kwa ajili yako"

mkimbizi na mtu asiye na makao

Unaweza kuunganisha maneno haya pamoja. "mkimbizi asiye na makao"