sw_tn/gen/01/06.md

972 B

Na kuwe na anga kati ya maji ...na ligawe

Hizi ni amri. Kwa kuamuru kwamba anga kati ya maji iwepo na igawe maji, Mungu alifanya iwepo na kugawa maji na maji.

anga

"anga tupu na wazi". Watu wa Kiyahudi walichukulia uwazi huu kuwa na umbo kama la kuba au bakuli lililofunikwa.

kati ya maji

"ndani ya maji"

Mungu alifanya anga na kugawanya maji

"kwa namna hii, Mungu alifanya anga na kugawa maji." Mungu alipozungumza, ilitokea. Sentensi hii inaeleza kitu gani Mungu alifanya alipokuwa akizungumza.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya pili

Hii inamaanisha siku ya pili ambapo ulimwengu ulipoanza kuwepo.