sw_tn/act/11/19.md

858 B

Sentensi unganishi

Luka anaelezea kuhusu kile kilichotokea kwa waumini waliokimbia baada ya kuuawa kwa Stefano kwa mawe.

Sasa

Luka anatambulisha simlizi mpya

waamini ambao mateso yalianzia kwenye kifo cha Stephano walitawanyika kutoka Yerusalemu-waamini hawa walienda mbali,

Mateso yaliyoanza na kifo cha Stefano yalisababisha waumini kukimbia na kusambaa maeneo mbalimbali.

Wayahudi peke yake

Waumini walidhani ujumbe wa Mungu ulikuwa kwa ajili ya Wayahudi pekee na siyo kwa wamataifa pia.

na kusema na wayunani

Watu aliokuwa wakiongea kiyunana nao walikuwa ni watu wa mataifa hawakuwa Wayahudi.

Na mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao

Mkono wa Mungu unamaanisha nguvu zake. "Mungu alikuwa na nguvu kuwawezesha wale waumini kuhubiri kwa ujasiri".

na kumgeukia Bwana

Wengi waliacha kuiamini miungu yao ya zamani, na walimwamini Yesu.