sw_tn/act/05/38.md

743 B

Sentensi unganishi:

Gamarieli anamaliza kuwaeleza wajumbe wa baraza. Pamoja na kuwapiga wale mitume na kuwaamuru wasizidi kunena habari za Yesu na kuwaachia huru, lakini wanafunzi walizidi kufundisha na kuhubiri habari za Yesu.

jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe,

Gamalieli anawaambia Wayahudi viongozi wasiwaadhibu hao mitume na wasiwatie tena gerezani.

kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa

Kama jambo hili wanalolitenda chimbuko lake ni mwanadamu litakoma tu.

Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia

Kama kazi hii wanayoifanya chimbuko lake ni Mungu, kazi hii itaendelea.

Hivyo, walishawishika na maneno yake.

Gamalieli alifanikiwa kuwashawishi Viongozi Wayahudi na kukubaliana na ushawishi wake.