sw_tn/2sa/14/12.md

823 B

sema neno zaidi

"kusema nawe neno zaidi." Mwanamke anaomba kusema na mfalme jambo lingine.

Mtumishi wako

Kuonesha heshima kwa mfalme

Kuongea zaidi

Mfalme alimpa ruhusu kuongea zaidi.

Kwa nini basi umetenda jambo la namna hiyo kwa watu wa Mungu?

Mwanamke anauliza swali hili kumkemea Daudi kwa jinsi alivyomtendea Absalomu.

Mfalme ni kama mwenye hatia

Mwanamke anamlinganisha mfalme na mtu mwingine aliye na hatia bila kusema moja kwa moja.

Mwanawe aliyefukuzwa

Hii inaweza kuelezwa kama "mwanawe aliyetengwa.

Maana wote ni lazima tufe, nasi ni kama maji tukimwagika juu ya ardhi... juu tena.

Hapa mwanamke anazungumzia mtu anayekufa kama maji yamwagikayo juu ya nchi.

Mungu... hutafuta njia kwa wale waliofukuzwa kurudishwa tena.

Mwanamke anaonesha kwamba Daudi anapaswa kumrudisha mwanawe.