sw_tn/2sa/11/06.md

657 B

Kisha Daudi akatuma

Hapa neno "kutuma" inamaanisha kwamba Daudi alituma mjumbe.

Yoabu anaendeleaje, jeshi linaendeleaje, na vita inaendeleaje

Daudi alikuwa akiuliza ikiwa Yoabu na jeshi walikuwa wanaendelea vema na kuhusu maendeleo ya vita.

Shuka nyumbani kwako

Maana pendekezwa kwa kifungu "shuka chini" ni 1) Nyumba ya Uria ilikuwa chini kuliko kasiri la Daudi au 2) Nyumba ya Uria ilikuwa na umuhimu mdogo kulinganisha na kasiri la mfalme.

Nawa miguu yako

Kifungu hiki kinamaanisha kurudi nyumbani kupumzika wakati wa usiku baada ya kufanya kazi mchana kutwa.

Mfalme alituma zawadi kwa Uria

Daudi alituma mtu kupeleka zawadi kwa Uria.