sw_tn/2sa/07/08.md

1.0 KiB

Maelezo kwa Jumla

Yahwe anafafanua ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Basi

Hii haimaanishi "sasa," lakini imetumika kuonesha utayari kwa jambo mhimu lifuatalo.

mwambie mtumishi wangu Daudi, "Hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi: 'nilikutoa...jina kuu kwa ajili yako, kama jina la wakuu waliopo juu ya nchi.

Hii inanukuu ndani ya nukuu. Yaweza kufasiriwa: "mwambie Daudi mtumishi wangu kwamba nilimtoa... jina kuu kwa ajili yake, kama jina la mojawapo wa watu wakuu waliopo duniani"

mwambie Daudi mtumishi wangu

Yahwe bado anamwambia nabii Nathani anachopaswa kumwambia Daudi.

nimekuwa pamoja nawe

Hapa "pamoja nawe" inamaanisha kwamba Yahwe amemsaidia na kumbariki Daudi.

na nimewaondoa adui zako wote

Yahwe aliwaaribu adui wa Daudi inazungumzwa kana kwamba Yahwe aliowaondolea mbali, kama ambavyo mtu angekata vipande vya nguo au tawi kutoka katika mti.

kufanya jina kuu kwa ajili yako

Hapa "jina" inawakilisha heshima ya mtu.

kama jina la wakuu waliopo duniani

Kifungu "wakuu" inamaanisha watu mashuhuri.