forked from WA-Catalog/sw_tn
1.0 KiB
1.0 KiB
Maelezo kwa Jumla
Yahwe anafafanua ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.
Basi
Hii haimaanishi "sasa," lakini imetumika kuonesha utayari kwa jambo mhimu lifuatalo.
mwambie mtumishi wangu Daudi, "Hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi: 'nilikutoa...jina kuu kwa ajili yako, kama jina la wakuu waliopo juu ya nchi.
Hii inanukuu ndani ya nukuu. Yaweza kufasiriwa: "mwambie Daudi mtumishi wangu kwamba nilimtoa... jina kuu kwa ajili yake, kama jina la mojawapo wa watu wakuu waliopo duniani"
mwambie Daudi mtumishi wangu
Yahwe bado anamwambia nabii Nathani anachopaswa kumwambia Daudi.
nimekuwa pamoja nawe
Hapa "pamoja nawe" inamaanisha kwamba Yahwe amemsaidia na kumbariki Daudi.
na nimewaondoa adui zako wote
Yahwe aliwaaribu adui wa Daudi inazungumzwa kana kwamba Yahwe aliowaondolea mbali, kama ambavyo mtu angekata vipande vya nguo au tawi kutoka katika mti.
kufanya jina kuu kwa ajili yako
Hapa "jina" inawakilisha heshima ya mtu.
kama jina la wakuu waliopo duniani
Kifungu "wakuu" inamaanisha watu mashuhuri.