sw_tn/2sa/07/06.md

944 B

Je niliwai kusema jambo lolote kwa kiongozi yeyote wa Israeli niliyemchagua kuwachunga watu wangu Israeli, kusema, "Kwa nini hamjanijengea nyumba ya mwerezi?

Hii ina nukuu ndani ya nukuu nyingine. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. Yaani: "Sijawai kumwambia mmojawapo wa viongozi, niliowachagua, kunijengea hekalu la mbao za mwerezi."

Je niliwai kusema jambo lolote kwa kiongozi yeyote wa Israeli

Yahwe anatumia nukuu kusisitiza kwamba hakuwai kuwambia viongozi wa Israeli kumjengea nyumba.

Kwa nini hamkuwai kunijengea nyumba ya mwerezi?

Ikiwa Yahwe alikuwa amewauliza viongozi swali hili, angekuwa ametumia swali kuwalaumu kwa kutomjengea nyumba ya mwerezi. Lakini, Yahwe alisema hapo mwanzo kwamba hakuwa amewauliza swali hili. Yaani: "Mlipaswa kuwa mmenijengea nyumba ya mwerezi."

niliowateua kuwachunga watu wangu Israeli

Viongozi wanasemwa kama wachungaji na watu kama kondoo.