sw_tn/2sa/06/08.md

462 B

Peresi Uza

Hili ni jina la mahali. Mtu anayetafasiri anaweza kuongeza maelezo ya chini kusema, "Jina Peresi Uza linamaanisha 'adhabu ya Uza."'

hadi siku hiyo

Hii inamaanisha hadi wakati habari hii ilipokuwa inaandikwa, siyo sasa katika karne ya ishirini na moja.

Jinsi gani sanduku la Yahwe lije kwangu?

Daudi anatumia swali hili kusisitiza kwamba anaogopa kulipeleka sanduku Yerusalem. Yaani: "Ninaogopa sana kulileta sanduku la Yahwe Yerusalemu."