sw_tn/2sa/02/26.md

1.1 KiB

Kuita

"piga kelele"

Ni lazima upanga urarue daima?

Swali hili linasisitiza kwamba vita ilikuwa imeendelea muda mrefu. Hapa "upanga" inaonesha mapigano. Mauaji katika vita yanaoneshwa kama mnyama wa mwituni anakula askari. Inamaanisha pia "Hatuitaji kutumia kupigana na kuuana."

Je haujui kwamba itakuwa uchungu mwishowe?

Swali linatumika kumlazimisha Yoabu kukubari kwamba kuendelea kupigana kungeishia maafa makubwa. Hapa "uchungu" ni neno lililotumika kuonesha matesa makali ambayo yangetukia.

Je hata lini utawazuia watu wako wasiwafuatie ndugu zao.

Swali hili linakusudiwa kumshawishi Yoabu kuacha kupigana na Waisraeli wenzake. Hapa "ndugu" inawakilisha watu wa taifa la Israeli. Yaani "Acha sasa jambo hili ili Waisraeli wasiendelee kuuana.

kama Mungu aishivyo

Hiki ni kiapo kikubwa sana. Inamaana ya "pamoja na Mungu kama shahidi wangu" au "Mungu anathibitisha kuwa namaanisha ninachosema."

kama usingesema hivyo...kuwafuatia ndugu zao hata asubuhi

Taarifa hii ya kukisia inaongelea ambacho kingetokea kama Abneri asingemwambia Yoabu kwa hekima.