sw_tn/2sa/01/25.md

1.0 KiB

Jinsi wenye uwezo walivyoanguka

Kifungu hiki kinajirudia katika mstari wa 25 na 27 kusistiza kwamba mashujaa hodari wa Israeli wamekufa. Inaweza pia kuwa "Watu wenye uwezo wamekufa vitani.

wenye nguvu

"nguvu" hapa ina wingi na inaweza kumhusu Sauli na Yonathani pekee, au askari wote wa Israeli. Inaweza pia kuwa mashujaa wenye nguvu.

wameanguka

hii ni njia laini ya kusema "wamekufa vitani."

Yonathani amekufa

Hii inaweza kutaarifiwa katika kauli tendaji. Yaani "Yonathani amekufa vitani" au adui amemwua Yonathani"

Juu ya mahali pako pa juu

Daudi anaendelea kuielekeza sehemu hii ya wimbo katika milima ya Gilboa kama alivyoanza katika 1:21.

Yonathani ndugu yangu

"ndugu" hapa imetumika katika hali ya urafiki wa karibu sana.

Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, kupita upendo wa wanawake.

Hapa "upendo" umetumika katika hali ya urafiki na uaminifu. Uaminifu wa Yonathani kwa Daudi ulikuwa mkuu kuliko uaminifu alionao mwanamke kwa mmewew na watoto.

silaha za vita zimeangamizwa

"silaha zao zimeharibiwa"