forked from WA-Catalog/sw_tn
28 lines
1.1 KiB
Markdown
28 lines
1.1 KiB
Markdown
|
# Usiwe na hofu, Mariamu
|
||
|
|
||
|
Malaika hakutaka Mariamu kuwa na woga kwa ujio wake, kwasababu Mungu alimtuma ujumbe mzuri.
|
||
|
|
||
|
# umepata wema wa Mungu
|
||
|
|
||
|
Nahau "kupata fadhila" inamaana kupokelewa vizuri na mtu fulani. Sentensi inaweza kugeuzwa kuonesha Mungu kama mtenda. NI: "Mungu ameamua kutoa neema yake" au "Mungu anaonesha wema wake."
|
||
|
|
||
|
# utakuwa na ujauzito tumboni mwako na kuzaa mwana ... Yesu ... Mwana wa aliye Juu Sana
|
||
|
|
||
|
Mariamu atazaa "mwana" atakayeitwa "Mtoto wa aliye Juu Sana" (UDB). Yesu ni mtoto aliyezaliwa na mama mwanadamu, na Yeye vilevile ni Mwana wa Mungu. Maneno haya yatafsiriwe kwa uanglifu sana.
|
||
|
|
||
|
# ataitwa
|
||
|
|
||
|
Maana zinazowezekana ni 1) "watu watamwita" au 2) "Mungu atamwita."
|
||
|
|
||
|
# Mwana wa aliye Juu Sana
|
||
|
|
||
|
Hii ni sifa mhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.
|
||
|
|
||
|
# Kupewa kiti cha mhenga wake Daudi
|
||
|
|
||
|
Kiti kinawakilisha mamlaka ya mfalme kutawala. NI: "kumpa mamlaka kutawala kama mfalme kama baba yake Daudi alivyofanya"
|
||
|
|
||
|
# hapatakuwa na mwisho kwa ufalme wake
|
||
|
|
||
|
Kauli hasi ""hakuna mwisho" sisitiza kwamba utaendelea milele. Pia inaweza kusemwa kwa kauli chanya. NI: "ufalme wake hautaisha."
|