\v 3 Sikilizeni! Sauti ya kilio kikuu inakuja kutoka Horonaimu, ambako kuna maafa na maangamizi makuu. \v 4 Moabu ameangamizwa. Watoto wake wamesikika kwa sauti za vilio vyao. \v 5 Wanapanda kilima cha Luhithi wakilia, kwani njia yote kuteremkia Horonaimu, vilio vinasikika kutokana na maangamizi.