sw_tw/bible/other/bow.md

1.2 KiB

Kuinama chini

Ufafanuzi

Kuinama maana yake kujikunja kwa unyenyekevu kuonesha heshima kwa mtu. "Kuinama chini" inamaanisha kupiga magoti chini sana, kwa kawaida uso na mikono ikielekea ardhini.

  • Viashiria vingine ni pamoja na "kupiga goti" na "kuinamisha kichwa"( maana yake ni kuinamisha kichwa mbele kwa heshima ya unyenyekevu au katika huzuni).
  • Kuinama chini pia kwaweza kuwa ishara ya mfadhaiko au maombolezo. Mtu "anayeinamishwa chini" amewekwa katika kiwango cha chini sana cha unyenyekevu.
  • Kwa kawaida mtu atainama mbele ya mtu mwenye heshima ya juu kuliko yake au mwenye umuhimu mkubwa, kama wafalme na viongozi wengine.
  • Kuinama mbele ya Mungu ni ishara ya kumwabudu.
  • Katika Biblia, watu walimwinamia Yesu walipotambua kutokana na miujiza yake na mafundisho yake kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu.
  • Biblia inasema kwamba Yesu atakaporudi, kila mtu atapiga goti kumwabudu.

Maoni ya Kutafasiri

  • Kwa kutegemea na mazingira, neno hili laweza kutafasiriwa kwa neno au kifungu kinachomaanisha, "kuinamia" au "kuinamisha kichwa" au "piga goti".
  • Neno "inama chini" laweza kutafasiriwa kama "Piga magoti" au "jinyenyekesha".
  • Baadhi ya lugha zitakuwa na njia zaidi ya moja ya kutafasiri neno hili, kutegemea na mazingira.