sw_tw/bible/names/babel.md

692 B

Babeli

Ufafanuzi

Babeli ulikuwa mji mkuu katika eneo lililoitwa Shinari kusini mwa Mesopotamia. Shinari ulikuja baadaye kuitwa Babiloni.

  • Mji wa Babeli ulianzishwa na Nimrodi, mjukuu wa Hamu, aliyemiliki eneo la Shinari.
  • Watu wa Shinari hatimaye wakawa na kiburi kwa kuamua kujenga mnara mrefu wa kuweza kufika mbinguni. Baada ulijulikana kama "Mnara wa Babeli."
  • Kwa kuwa kwa kujenga mnara watu walikataa kutawanyika kama Mungu alivyokuwa ameagiza, yeye alichanganya lugha zao ili wasielewane. Hii iliwalazimisha kuondoka na kwenda kuishi maeneo mbalimbali ya dunia.
  • Kiini cha maana ya neno "Babeli" ni "machafuko," likitokana na wakati Mungu alipochanganya lugha ya watu.