sw_tn/act/22/intro.md

1.4 KiB

Matendo 22 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Hii ndio mara ya pili kusema habari ya Kubadilishwa kwa Paulo kuwa Mkristo katika kitabu cha Matendo.Kwa sababu hili ni tukio muhimu katika kanisa la awali, "kuna mara tatu ya kusema habari ya kubadilishwa kwa Paulo kuwa Mkristo. (Tazama: Matendo 9 na Matendo 26).

Dhana maalum katika sura hii

Katika lugha ya Kihebrania

Wakati huu Wayahudi wengi walizungumza Kiaramea na Kiyunani. Wengi wa waliozungumza Kihebrania walikuwa Wayahudi watu wa elimu. Hii ndio maana watu walimsikiliza Paulo kwa makini alipoanza kuzungumza kwa Kihebrania.

"The Way"

Hakuna anayefahamu aliyeanza kuwaita Waumini wafuasi wa Njia. Labda Waumini walijiita hivyo kwa vile Bibilia kwa mara nyingi humzungumzia mtu anayeishi maishi yake kama mtu atembeaye njiani. Kama huu ni ukweli, Waumini walikuwa "Wakifuata njia ya Bwana" kwa kuishi kwa njia inayompendeza Mungu.

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani Kwmaba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamoja walizaliwa raia wa Roma na wengine wakalipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia. "Kiranja Mkuu" angeadhibiwa kwa kuwatendea raia wa Urumi sawa wale wasiokuwa raia.

<< | >>