sw_tn/rev/22/12.md

881 B

Taarifa ya Jumla:

Kitabu cha Ufunuo kikiwa kinafika mwisho, Yesu anatoa salamu zake za kufunga.

Alfa na Omega, wa Kwanza na wa Mwisho, Mwanzo na Mwisho

Misemo hii mitatu inafanana maana na inasisitiza kuwa Yesu alikuwepo na ataendelea kuwepo muda wote.

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". Kama haieleweki kwa wasomaji unaweza kufikiria kutumia herufi katika alfabeti zako. "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

wa Kwanza na wa Mwisho

Hii inamaanisha uasili wa Yesu wa milele.

Mwanzo na Mwisho

Maana zinazowezekana ni 1)"yule aliyeanzisha vitu vyote na ambaye atasababisha vyote kufika mwisho" (UDB) au 2) "yule aliyekuwepo kabla ya vitu vyote na atakuwepo baada ya vitu vyote."