sw_tn/rev/21/03.md

617 B

Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema

Neno "sauti" inamaanisha yule anayezungumza. "mtu akinena kwa sauti kutoka katika kiti cha enzi akisema"

Tazama!

Nenno "Tazama" inatuweka macho kuwa makini na taarifa za kushangaza zifuatazo.

Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza kuwa, hakika, Mungu ataishi miongoni mwa watu.

Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao

Machozi hapa yanawakilisha huzuni. "Mungu atafuta huzuni yao kama vile anafuta machozi yao" au "Mungu atawasababisha wasiwe na huzuni tena"